Psalms 96
1Mwimbieni Bwana wimbo mpya; 2 mwimbieni Bwana dunia yote. 1
2Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; 2 tangazeni wokovu wake siku baada ya siku. 1
3Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, 2 matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote. 1
4Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; 2 yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote. 1
5Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, 2 lakini Bwana aliziumba mbingu. 1
6Fahari na enzi viko mbele yake; 2 nguvu na utukufu vimo patakatifu pake. 1
7Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, 2 mpeni Bwana utukufu na nguvu. 1
8Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; 2 leteni sadaka na mje katika nyua zake. 1
9Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; 2 dunia yote na itetemeke mbele zake. 1
10Katikati ya mataifa semeni, “ Bwana anatawala.” 1 Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; 2 atawahukumu watu kwa uadilifu. 1
11Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; 2 bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake; 1
12mashamba na yashangilie, 2 pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. 1 Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha; 2
13itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, 2 anakuja kuihukumu dunia. 1 Ataihukumu dunia kwa haki, 2 na mataifa katika kweli yake.