Psalms 135
1Msifuni Bwana. 1 Lisifuni jina la Bwana, 2 msifuni, enyi watumishi wa Bwana, 1
2ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, 2 katika nyua za nyumba ya Mungu wetu. 1
3Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, 2 liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza. 1
4Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, 2 Israeli kuwa mali yake ya thamani. 1
5Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, 2 kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote. 1
6Bwana hufanya lolote apendalo, 2 mbinguni na duniani, 2 katika bahari na vilindi vyake vyote. 1
7Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; 2 hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua 2 na huleta upepo kutoka ghala zake. 1
8Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, 2 mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama. 1
9Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, 2 dhidi ya Farao na watumishi wake wote. 1
10Aliyapiga mataifa mengi, 2 na akaua wafalme wenye nguvu: 1
11Mfalme Sihoni na Waamori, 2 Ogu mfalme wa Bashani 2 na wafalme wote wa Kanaani: 1
12akatoa nchi yao kuwa urithi, 2 urithi kwa watu wake Israeli. 1
13Ee Bwana, jina lako ladumu milele, 2 kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote. 1
14Maana Bwana atawathibitisha watu wake, 2 na kuwahurumia watumishi wake. 1
15Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, 2 zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu. 1
16Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, 2 zina macho, lakini haziwezi kuona; 1
17zina masikio, lakini haziwezi kusikia, 2 wala hakuna pumzi katika vinywa vyao. 1
18Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, 2 vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia. 1
19Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; 2 ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana; 1
20ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; 2 ninyi mnaomcha, msifuni Bwana. 1
21Msifuni Bwana kutoka Sayuni, 2 msifuni yeye aishiye Yerusalemu. 1 Msifuni Bwana.