Psalms 20
1Bwana na akujibu unapokuwa katika dhiki, 2 jina la Mungu wa Yakobo na liwe kinga yako. 1
2Na akutumie msaada kutoka patakatifu 2 na akupatie msaada kutoka Sayuni. 1
3Na azikumbuke dhabihu zako zote, 2 na azikubali sadaka zako za kuteketezwa. 1
4Na akujalie haja ya moyo wako, 2 na aifanikishe mipango yako yote. 1
5Tutashangilia kwa furaha utakaposhinda, 2 tutainua bendera zetu kwa jina la Mungu wetu. 1 Bwana na akupe haja zako zote. 1
6Sasa nafahamu kuwa Bwana 2 humwokoa mpakwa mafuta wake, 1 humjibu kutoka mbingu yake takatifu 2 kwa nguvu za wokovu wa mkono wake wa kuume. 1
7Wengine wanatumaini magari ya vita, na wengine farasi, 2 bali sisi tutalitumainia jina la Bwana, Mungu wetu. 1
8Wao wameshushwa chini na kuanguka, 2 bali sisi tunainuka na kusimama imara. 1
9Ee Bwana, mwokoe mfalme! 2 Tujibu tunapokuita!