Psalms · Biblia (Kiswahili)

Psalms 65

1Ee Mungu, sifa zakungojea katika Sayuni; 2 kwako wewe nadhiri zetu zitatimizwa. 1

2Ewe usikiaye maombi, 2 kwako wewe watu wote watakuja. 1

3Tulipokuwa tumefunikwa kabisa na dhambi, 2 wewe ulisamehe makosa yetu. 1

4Heri wale uliowachagua 2 na kuwaleta karibu ili waishi katika nyua zako! 1 Tunashibishwa kwa mema ya nyumba yako, 2 mema ya Hekalu lako takatifu. 1

5Unatujibu kwa matendo ya kushangaza ya haki, 2 Ee Mungu Mwokozi wetu, 1 tumaini la miisho yote ya duniani 2 na la bahari zilizo mbali sana, 1

6uliyeumba milima kwa uwezo wako, 2 ukiwa umejivika nguvu, 1

7uliyenyamazisha dhoruba za bahari, 2 ngurumo za mawimbi yake, 2 na ghasia za mataifa. 1

8Wale wanaoishi mbali sana 2 wanaogopa maajabu yako, 1 kule asubuhi ipambazukiapo 2 na kule jioni inakofifilia 2 umeziita nyimbo za furaha. 1

9Waitunza nchi na kuinyeshea, 2 waitajirisha kwa wingi. 1 Vijito vya Mungu vimejaa maji 2 ili kuwapa watu nafaka, 2 kwa maana wewe umeviamuru. 1

10Umeilowesha mifereji yake 2 na kusawazisha kingo zake; 1 umeilainisha kwa manyunyu 2 na kuibariki mimea yake. 1

11Umeuvika mwaka taji ya baraka, 2 magari yako yanafurika kwa wingi. 1

12Mbuga za majani za jangwani umezineemesha; 2 vilima vimevikwa furaha. 1

13Penye nyanda za malisho pamejaa makundi ya wanyama, 2 na mabonde yamepambwa kwa mavuno; 2 vyote vinashangilia kwa furaha na kuimba.

← Psalms 64Read In The App, Free →Psalms 66 →

Study Psalms 65

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschCharles SpurgeonScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150