Psalms 97
1Bwana anatawala, nchi na ifurahi, 2 visiwa vyote vishangilie. 1
2Mawingu na giza nene vinamzunguka, 2 haki na hukumu ndio msingi wa kiti chake cha enzi. 1
3Moto hutangulia mbele zake 2 na huteketeza adui zake pande zote. 1
4Umeme wake wa radi humulika dunia, 2 nchi huona na kutetemeka. 1
5Milima huyeyuka kama nta mbele za Bwana, 2 mbele za Bwana wa dunia yote. 1
6Mbingu zinatangaza haki yake, 2 na mataifa yote huona utukufu wake. 1
7Wote waabuduo sanamu waaibishwa, 2 wale wajisifiao sanamu: 2 mwabuduni yeye, enyi miungu yote! 1
8Sayuni husikia na kushangilia, 2 vijiji vya Yuda vinafurahi 2 kwa sababu ya hukumu zako, Ee Bwana. 1
9Kwa kuwa wewe, Ee Bwana, ndiwe Uliye Juu Sana kuliko dunia yote; 2 umetukuka sana juu ya miungu yote. 1
10Wale wanaompenda Bwana na wauchukie uovu, 2 kwa maana yeye hulinda maisha ya waaminifu wake 2 na kuwaokoa kutoka mkononi mwa mwovu. 1
11Nuru huangaza wenye haki 2 na furaha kwa watu wanyofu wa moyo. 1
12Furahini katika Bwana, ninyi mlio wenye haki, 2 lisifuni jina lake takatifu.