Psalms 12
1Bwana tusaidie, kwa kuwa wacha Mungu wametoweka; 2 waaminifu wametoweka miongoni mwa wanadamu. 1
2Kila mmoja humwambia jirani yake uongo; 2 midomo yao ya hila huzungumza kwa udanganyifu. 1
3Bwana na akatilie mbali midomo yote ya hila 2 na kila ulimi uliojaa majivuno, 1
4ule unaosema, “Kwa ndimi zetu tutashinda; 2 midomo ni mali yetu, bwana wetu ni nani?” 1
5“Kwa sababu ya uonevu wa wanyonge 2 na kulia kwa uchungu kwa wahitaji, 1 nitainuka sasa,” asema Bwana. 2 “Nitawalinda kutokana na wale 2 wenye nia mbaya juu yao.” 1
6Maneno ya Bwana ni safi, 2 kama fedha iliyosafishwa katika tanuru, 2 iliyosafishwa mara saba. 1
7Ee Bwana, utatuweka salama 2 na kutulinda na kizazi hiki milele. 1
8Watu waovu huenda wakiringa kila mahali 2 wakati ambapo yule aliye mbaya sana 2 ndiye anayeheshimiwa miongoni mwa watu.