Psalms 59
1Ee Mungu, uniokoe na adui zangu, 2 unilinde kutokana na hao wanaoinuka dhidi yangu. 1
2Uniponye na watu watendao mabaya, 2 uniokoe kutokana na wamwagao damu. 1
3Tazama wanavyonivizia! 2 Watu wakali wananifanyia hila, 1 ingawa Ee Bwana, mimi sijakosea 2 wala kutenda dhambi. 1
4Sijatenda kosa; hata hivyo wako tayari kunishambulia. 2 Inuka unisaidie, uone hali yangu mbaya! 1
5Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli! 2 Zinduka uyaadhibu mataifa yote, 2 usionyeshe huruma kwa wasaliti. 1
6Hurudi wakati wa jioni, 2 wakibweka kama mbwa, 2 wakiuzurura mji. 1
7Tazama yale wanayotema kutoka vinywa vyao, 2 hutema upanga kutoka midomo yao, 2 nao husema, “Ni nani atakayetusikia?” 1
8Lakini wewe, Bwana, uwacheke; 2 unayadharau mataifa hayo yote. 1
9Ee nguvu yangu, ninakutazama wewe, 2 wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu, 2
10Mungu wangu unipendaye. 1 Mungu atanitangulia, 2 naye atanifanya niwachekelee 2 wale wanaonisingizia. 1
11Lakini usiwaue, Ee Bwana, ngao yetu, 2 au sivyo watu wangu watasahau. 1 Katika uwezo wako wafanye watangetange 2 na uwashushe chini. 1
12Kwa ajili ya dhambi za vinywa vyao, 2 kwa ajili ya maneno ya midomo yao, 2 waache wanaswe katika kiburi chao. 1 Kwa ajili ya laana na uongo wanaotamka, 2
13wateketeze katika ghadhabu, 2 wateketeze hadi wasiwepo tena. 1 Ndipo itakapofahamika katika miisho ya dunia 2 kwamba Mungu anatawala juu ya Yakobo. 1
14Hurudi jioni, 2 wakibweka kama mbwa, 2 wakiuzurura mji. 1
15Wanatangatanga wakitafuta chakula, 2 wasipotosheka hubweka kama mbwa. 1
16Lakini mimi nitaziimba nguvu zako, 2 asubuhi nitaimba juu ya upendo wako; 1 kwa maana wewe ndiwe ngome yangu 2 na kimbilio langu wakati wa shida. 1
17Ee uliye Nguvu zangu, ninakuimbia sifa. 2 Wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu, 2 Mungu unipendaye.