Psalms 72
1Ee Mungu, mjalie mfalme aamue kwa haki yako, 2 mwana wa mfalme kwa haki yako. 1
2Atawaamua watu wako kwa haki, 2 watu wako walioonewa kwa haki. 1
3Milima italeta mafanikio kwa watu, 2 vilima tunda la haki. 1
4Atawatetea walioonewa miongoni mwa watu 2 na atawaokoa watoto wa wahitaji, 2 ataponda mdhalimu. 1
5Atadumu kama jua lidumuvyo, kama mwezi, vizazi vyote. 1
6Atakuwa kama mvua inyeshayo juu ya shamba lililofyekwa, 2 kama manyunyu yanyeshayo ardhi. 1
7Katika siku zake wenye haki watastawi; 2 mafanikio yatakuwepo mpaka mwezi utakapokoma. 1
8Atatawala kutoka bahari hadi bahari 2 na kutoka Mto + 72:8 Yaani Mto Frati. mpaka miisho ya dunia. 1
9Makabila ya jangwani watamsujudia, 2 na adui zake wataramba mavumbi. 1
10Wafalme wa Tarshishi na wa pwani za mbali 2 watamletea kodi; 1 wafalme wa Sheba na Seba 2 watampa zawadi. 1
11Wafalme wote watamsujudia 2 na mataifa yote yatamtumikia. 1
12Kwa maana atamwokoa mhitaji anayemlilia, 2 aliyeonewa asiye na wa kumsaidia. 1
13Atawahurumia wanyonge na wahitaji 2 na kuwaokoa wahitaji kutoka mauti. 1
14Atawaokoa kutoka uonevu na ukatili, 2 kwani damu yao ni ya thamani machoni pake. 1
15Aishi maisha marefu! 2 Na apewe dhahabu ya Sheba. 1 Watu wamwombee daima 2 na kumbariki mchana kutwa. 1
16Nafaka ijae tele katika nchi yote, 2 juu ya vilele vya vilima na istawi. 1 Tunda lake na listawi kama Lebanoni, 2 listawi kama majani ya kondeni. 1
17Jina lake na lidumu milele, 2 na lidumu kama jua. 1 Mataifa yote yatabarikiwa kupitia kwake, 2 nao watamwita aliyebarikiwa. 1
18Bwana Mungu, Mungu wa Israeli, apewe sifa, 2 yeye ambaye peke yake hutenda mambo ya ajabu. 1
19Jina lake tukufu lisifiwe milele, 2 ulimwengu wote ujae utukufu wake. Amen na Amen. 1
20Huu ndio mwisho wa maombi ya Daudi mwana wa Yese.