Psalms 29
1Mpeni Bwana, enyi mashujaa, 2 mpeni Bwana utukufu na nguvu. 1
2Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; 2 mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake. 1
3Sauti ya Bwana iko juu ya maji; 2 Mungu wa utukufu hupiga radi, 2 Bwana hupiga radi juu ya maji makuu. 1
4Sauti ya Bwana ina nguvu; 2 sauti ya Bwana ni tukufu. 1
5Sauti ya Bwana huvunja mierezi; 2 Bwana huvunja vipande vipande 2 mierezi ya Lebanoni. 1
6Hufanya Lebanoni irukaruke kama ndama, 2 Sirioni + 29:6 Yaani Mlima Hermoni. urukaruke kama mwana nyati. 1
7Sauti ya Bwana hupiga kwa miali 2 ya umeme wa radi. 1
8Sauti ya Bwana hutikisa jangwa; 2 Bwana hutikisa Jangwa la Kadeshi. 1
9Sauti ya Bwana huzalisha ayala, 2 na huuacha msitu wazi. 1 Hekaluni mwake wote wasema, 2 “Utukufu!” 1
10Bwana huketi akiwa ametawazwa juu ya gharika; 2 Bwana ametawazwa kuwa Mfalme milele. 1
11Bwana huwapa watu wake nguvu; 2 Bwana huwabariki watu wake kwa kuwapa amani.