Psalms 31
1Ee Bwana, nimekukimbilia wewe, 2 usiache nikaaibika kamwe, 2 kwa haki yako uniokoe. 1
2Nitegee sikio lako, 2 uje uniokoe haraka; 1 uwe kwangu mwamba wa kimbilio, 2 ngome imara ya kuniokoa. 1
3Kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu, 2 uniongoze na kunilinda kwa ajili ya jina lako. 1
4Uniepushe na mtego niliotegewa, 2 maana wewe ndiwe kimbilio langu. 1
5Ninaikabidhi roho yangu mikononi mwako, 2 unikomboe Ee Bwana, uliye Mungu wa kweli. 1
6Ninawachukia wale wanaongʼangʼania sanamu batili; 2 mimi ninamtumaini Bwana. 1
7Nitafurahia na kushangilia upendo wako, 2 kwa kuwa uliona mateso yangu 2 na ulijua maumivu ya nafsi yangu. 1
8Hukunikabidhi kwa adui yangu 2 bali umeiweka miguu yangu mahali penye nafasi. 1
9Ee Bwana unihurumie, kwa kuwa niko kwenye shida; 2 macho yangu yanafifia kwa huzuni, 2 nafsi yangu na mwili wangu kwa sikitiko. 1
10Maisha yangu yamedhoofika kwa majonzi, 2 naam, miaka yangu kwa kulia kwa maumivu makali; 1 nguvu zangu zinaisha kwa ajili ya mateso, 2 na mifupa yangu inachakaa. 1
11Kwa sababu ya adui zangu wote, 2 nimedharauliwa kabisa na jirani zangu, 1 hata kwa rafiki zangu nimekuwa tisho, 2 wale wanionao barabarani hunikimbia. 1
12Nimesahaulika miongoni mwao kama mtu aliyekufa, 2 nimekuwa kama chombo cha mfinyanzi kilichovunjika. 1
13Kwa maana nimesikia maneno niliyosingiziwa na wengi; 2 vitisho viko pande zote; 1 kwa kuwa wamefanya mashauri dhidi yangu, 2 na kula njama kuniua. 1
14Lakini mimi ninakutumaini wewe peke yako, Ee Bwana; 2 nimesema, “Wewe ndiwe Mungu wangu.” 1
15Siku za maisha yangu ziko mikononi mwako, 2 uniokoe mikononi mwa adui zangu 2 na wale wanifuatiao. 1
16Mwangazie mtumishi wako uso wako, 2 uniokoe kwa ajili ya upendo wako usiokoma. 1
17Usiniache niaibike, Ee Bwana, 2 kwa maana nimekulilia wewe, 1 bali waovu waaibishwe 2 na kunyamazishwa Kuzimu. 1
18Midomo yao isemayo uongo na inyamazishwe, 2 kwa maana kwa kiburi na dharau 1 wao husema kwa majivuno 2 dhidi ya wenye haki. 1
19Tazama jinsi ulivyo mkuu wema wako, 2 uliowawekea akiba wakuchao, 1 ambao huwapa wale wakukimbiliao 2 machoni pa watu. 1
20Unawahifadhi katika uvuli wa uwepo wako 2 kutokana na hila za wanadamu; 1 katika makao yako huwaweka salama 2 kutokana na ndimi za mashtaka. 1
21Atukuzwe Bwana, 2 kwa kuwa amenionyesha upendo wake wa ajabu 2 nilipokuwa katika mji uliozingirwa. 1
22Katika hofu yangu nilisema, 2 “Nimekatiliwa mbali na macho yako!” 1 Hata hivyo ulisikia kilio changu 2 ukanihurumia nilipokuita unisaidie. 1
23Mpendeni Bwana ninyi watakatifu wake wote! 2 Bwana huwahifadhi waaminifu, 2 lakini wenye kiburi huwalipiza kikamilifu. 1
24Kuweni hodari na mjipe moyo, 2 ninyi nyote mnaomtumaini Bwana.