Psalms 2
1Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, 2 na kabila za watu kula njama bure? 1
2Wafalme wa dunia wanajipanga 2 na watawala wanajikusanya pamoja 1 dhidi ya Bwana 2 na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake. 1
3Wanasema, “Tuvunje minyororo yao 2 na kuvitupilia mbali vifungo vyao.” 1
4Yeye atawalaye mbinguni hucheka, 2 Bwana huwadharau. 1
5Kisha huwakemea katika hasira yake 2 na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema, 1
6“Nimemtawaza Mfalme wangu 2 juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.” 1 Ushindi Wa Mfalme 1
7Nitatangaza amri ya Bwana: 2 Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, 2 leo mimi nimekuzaa. 1
8Niombe, nami nitayafanya mataifa 2 kuwa urithi wako, 2 miisho ya dunia kuwa milki yako. 1
9Utawatawala kwa fimbo ya chuma 2 na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.” 1
10Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; 2 mwonyeke, enyi watawala wa dunia. 1
11Mtumikieni Bwana kwa hofu 2 na mshangilie kwa kutetemeka. 1
12Mbusu Mwana, asije akakasirika 2 nawe ukaangamizwa katika njia yako, 1 kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. 2 Heri wote wanaomkimbilia.