Psalms · Biblia (Kiswahili)

Psalms 63

1Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu, 2 nakutafuta kwa moyo wote; 1 nafsi yangu inakuonea kiu, 2 mwili wangu unakuonea wewe shauku, 1 katika nchi kame na iliyochoka 2 mahali ambapo hapana maji. 1

2Nimekuona katika mahali patakatifu 2 na kuuona uwezo wako na utukufu wako. 1

3Kwa sababu upendo wako ni bora kuliko uhai, 2 midomo yangu itakuadhimisha. 1

4Nitakusifu siku zote za maisha yangu, 2 na kwa jina lako nitainua mikono yangu. 1

5Nafsi yangu itatoshelezwa 2 kama kwa wingi wa vyakula; 1 kwa midomo iimbayo 2 kinywa changu kitakusifu wewe. 1

6Kitandani mwangu ninakukumbuka wewe, 2 ninawaza juu yako makesha yote ya usiku. 1

7Kwa sababu wewe ndiwe msaada wangu, 2 chini ya uvuli wa mbawa zako naimba. 1

8Nafsi yangu inaambatana nawe, 2 mkono wako wa kuume hunishika. 1

9Wale wanaotafuta uhai wangu wataharibiwa, 2 watakwenda chini kwenye vilindi vya dunia. 1

10Watatolewa wafe kwa upanga, 2 nao watakuwa chakula cha mbweha. 1

11Bali mfalme atafurahi katika Mungu, 2 wale wote waapao kwa jina la Mungu watamsifu, 2 bali vinywa vya waongo vitanyamazishwa.

← Psalms 62Read In The App, Free →Psalms 64 →

Study Psalms 63

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschCharles SpurgeonScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150