Psalms 92
1Ni vyema kumshukuru Bwana 2 na kuliimbia jina lako, Ee Uliye Juu Sana, 1
2kuutangaza upendo wako asubuhi, 2 na uaminifu wako wakati wa usiku, 1
3kwa zeze yenye nyuzi kumi 2 na kwa sauti ya kinubi. 1
4Ee Bwana, kwa kuwa matendo yako yamenifurahisha, 2 nitaziimba kwa shangwe kazi za mikono yako. 1
5Ee Bwana, tazama jinsi yalivyo makuu matendo yako, 2 tazama jinsi yalivyo ya kina mawazo yako! 1
6Mjinga hafahamu, 2 mpumbavu haelewi, 1
7ingawa waovu huchipua kama majani 2 na wote watendao mabaya wanastawi, 2 wataangamizwa milele. 1
8Bali wewe, Ee Bwana, 2 utatukuzwa milele. 1
9Ee Bwana, hakika adui zako, 2 hakika adui zako wataangamia. 2 Wote watendao mabaya watatawanyika. 1
10Umeitukuza pembe + 92:10 Pembe inawakilisha nguvu. yangu kama ile ya nyati dume, 2 mafuta mazuri yamemiminwa juu yangu. 1
11Macho yangu yamewaona adui zangu wakishindwa, 2 masikio yangu yamesikia maangamizi ya adui zangu waovu. 1
12Wenye haki watastawi kama mtende, 2 watakuwa kama mwerezi wa Lebanoni, 1
13waliopandwa katika nyumba ya Bwana, 2 watastawi katika nyua za Mungu wetu. 1
14Wakati wa uzee watakuwa bado wanazaa matunda, 2 watakuwa wabichi tena wamejaa nguvu, 1
15wakitangaza, “ Bwana ni mkamilifu; 2 yeye ni Mwamba wangu, 2 na ndani yake hamna uovu.”