Psalms 32
1Heri mtu yule ambaye amesamehewa makosa yake, 2 ambaye dhambi zake zimefunikwa. 1
2Heri mtu yule ambaye Bwana 2 hamhesabii dhambi, 1 na ambaye rohoni mwake 2 hamna udanganyifu. 1
3Niliponyamaza, mifupa yangu ilichakaa 2 kwa kulia kwa maumivu makali mchana kutwa. 1
4Usiku na mchana 2 mkono wako ulinilemea, 1 nguvu zangu zilinyonywa 2 kama vile katika joto la kiangazi. 1
5Kisha nilikujulisha dhambi yangu 2 wala sikuficha uovu wangu. 1 Nilisema, “Nitaungama 2 makosa yangu kwa Bwana.” 1 Ndipo uliponisamehe 2 hatia ya dhambi yangu. 1
6Kwa hiyo kila mtu mcha Mungu akuombe 2 wakati unapopatikana, 1 hakika maji makuu yatakapofurika 2 hayatamfikia yeye. 1
7Wewe ndiwe mahali pangu pa kujificha, 2 utaniepusha na taabu 2 na kunizunguka kwa nyimbo za wokovu. 1
8Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; 2 nitakushauri na kukuangalia. 1
9Usiwe kama farasi au nyumbu 2 wasio na akili, 1 ambao ni lazima waongozwe kwa lijamu na hatamu 2 la sivyo hawatakukaribia. 1
10Mtu mwovu ana taabu nyingi, 2 bali upendo usio na kikomo wa Bwana 2 unamzunguka mtu anayemtumaini. 1
11Shangilieni katika Bwana na mfurahi, enyi wenye haki! 2 Imbeni, nyote mlio wanyofu wa moyo!