Psalms · Biblia (Kiswahili)

Psalms 148

1Msifuni Bwana. 1 Msifuni Bwana kutoka mbinguni, 2 msifuni juu vileleni. 1

2Msifuni, enyi malaika wake wote, 2 msifuni yeye, enyi jeshi lake lote la mbinguni. 1

3Msifuni yeye, enyi jua na mwezi, 2 msifuni yeye, enyi nyota zote zingʼaazo. 1

4Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu sana, 2 na ninyi maji juu ya anga. 1

5Vilisifu jina la Bwana 2 kwa maana aliamuru navyo vikaumbwa. 1

6Aliviweka mahali pake milele na milele, 2 alitoa amri ambayo haibadiliki milele. 1

7Mtukuzeni Bwana kutoka duniani, 2 ninyi viumbe vikubwa vya baharini na vilindi vyote vya bahari, 1

8umeme wa radi na mvua ya mawe, theluji na mawingu, 2 pepo za dhoruba zinazofanya amri zake, 1

9ninyi milima na vilima vyote, 2 miti ya matunda na mierezi yote, 1

10wanyama wa mwituni na mifugo yote, 2 viumbe vidogo na ndege warukao, 1

11wafalme wa dunia na mataifa yote, 2 ninyi wakuu na watawala wote wa dunia, 1

12wanaume vijana na wanawali, 2 wazee na watoto. 1

13Wote na walisifu jina la Bwana, 2 kwa maana jina lake pekee limetukuka, 2 utukufu wake uko juu ya nchi na mbingu. 1

14Amewainulia watu wake pembe, + 148:14 Pembe hapa inawakilisha mwenye nguvu, yaani mfalme. 2 sifa ya watakatifu wake wote, 2 ya Israeli, watu walio karibu na moyo wake. 1 Msifuni Bwana.

← Psalms 147Read In The App, Free →Psalms 149 →

Study Psalms 148

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschCharles SpurgeonScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150