Psalms 55
1Ee Mungu, sikiliza maombi yangu, 2 wala usidharau hoja yangu. 1
2Nisikie na unijibu. 1 Mawazo yangu yananisumbua na nimehangaishwa 1
3kwa sauti ya adui, 2 kwa kukaziwa macho na waovu, 1 kwa sababu wananiletea mateso juu yangu 2 na kunitukana kwa hasira zao. 1
4Moyo wangu umejaa uchungu, 2 hofu ya kifo imenishambulia. 1
5Woga na kutetemeka vimenizunguka, 2 hofu kuu imenigharikisha. 1
6Nilisema, “Laiti ningekuwa na mbawa za njiwa! 2 Ningeruka niende mbali kupumzika. 1
7Ningalitorokea mbali sana 2 na kukaa jangwani, 1
8ningaliharakisha kwenda mahali pa salama, 2 mbali na tufani kali na dhoruba.” 1
9Ee Bwana, uwatahayarishe waovu 2 na uwachanganyishie semi zao, 2 maana nimeona jeuri na ugomvi mjini. 1
10Usiku na mchana wanazunguka juu ya kuta zake, 2 uovu na dhuluma vimo ndani yake. 1
11Nguvu za uharibifu zinatenda kazi mjini, 2 vitisho na uongo haviondoki mitaani mwake. 1
12Kama aliyenitukana ni adui yangu, ningevumilia, 2 kama mtu mwovu angejiinua dhidi yangu, 2 ningejificha asinione. 1
13Kumbe ni wewe, mwenzangu, 2 mshiriki na rafiki yangu wa karibu, 1
14ambaye awali tulifurahia ushirika mzuri, 2 tulipokuwa tukienda na umati hekaluni mwa Mungu. 1
15Kifo na kiwajie adui zangu ghafula, 2 na washuke kuzimu wangali hai, 2 kwa maana uovu upo ndani yao. 1
16Lakini ninamwita Mungu, 2 naye Bwana huniokoa. 1
17Jioni, asubuhi na adhuhuri 2 ninalia kwa huzuni, 2 naye husikia sauti yangu. 1
18Huniokoa nikawa salama katika vita 2 vilivyopangwa dhidi yangu, 2 ingawa watu wengi hunipinga. 1
19Mungu anayemiliki milele, 2 atawasikia na kuwaadhibu, 1 watu ambao hawabadilishi njia zao, 2 wala hawana hofu ya Mungu. 1
20Mwenzangu hushambulia rafiki zake, 2 naye huvunja agano lake. 1
21Mazungumzo yake ni laini kama siagi, 2 hata hivyo vita vimo moyoni mwake. 1 Maneno yake ni mororo kuliko mafuta, 2 hata hivyo ni upanga mkali uliofutwa. 1
22Mtwike Bwana fadhaa zako, 2 naye atakutegemeza, 2 hatamwacha kamwe mwenye haki wake aanguke. 1
23Lakini wewe, Ee Mungu, 2 utawashusha waovu katika shimo la uharibifu. 1 Wenye kiu ya kumwaga damu na wenye hila, 2 hawataishi nusu ya siku zao. 1 Lakini mimi ninakutumaini wewe.