Psalms 18
1Nakupenda wewe, Ee Bwana, 2 nguvu yangu. 1
2Bwana ni mwamba wangu, 2 ngome yangu na mwokozi wangu, 1 Mungu wangu ni mwamba, 2 ambaye kwake ninakimbilia. 1 Yeye ni ngao yangu na pembe ya wokovu wangu, 2 ngome yangu. 1
3Ninamwita Bwana anayestahili kusifiwa, 2 nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu. 1
4Kamba za mauti zilinizunguka, 2 mafuriko ya maangamizi yalinilemea. 1
5Kamba za kuzimu zilinizunguka, 2 mitego ya mauti ilinikabili. 1
6Katika shida yangu nalimwita Bwana, 2 nilimlilia Mungu wangu anisaidie. 1 Kutoka hekaluni mwake alisikia sauti yangu, 2 kilio changu kikafika mbele zake, 2 masikioni mwake. 1
7Dunia ilitetemeka na kutikisika, 2 misingi ya milima ikatikisika, 2 vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika. 1
8Moshi ukapanda kutoka puani mwake, 2 moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, 1 makaa ya moto yawakayo 2 yakatoka ndani mwake. 1
9Akazipasua mbingu akashuka chini, 2 mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake. 1
10Alipanda juu ya kerubi akaruka, 2 akapaa juu kwa mbawa za upepo. 1
11Alifanya giza kuwa kitu chake cha kujifunika, 2 hema lake kumzunguka, 2 mawingu meusi ya mvua ya angani. 1
12Kutokana na mwanga wa uwepo wake 2 mawingu yalisogea, 1 ikanyesha mvua ya mawe 2 na umeme wa radi. 1
13Bwana alinguruma kutoka mbinguni, 2 sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika. 1
14Aliipiga mishale yake na kutawanya adui, 2 naam, umeme mwingi wa radi na kuwafukuza. 1
15Mabonde ya bahari yalifunuliwa, 2 na misingi ya dunia ikawa wazi 1 kwa kukaripia kwako, Ee Bwana, 2 kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwako. 1
16Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; 2 alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu. 1
17Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, 2 kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi. 1
18Walinikabili siku ya msiba wangu, 2 lakini Bwana alikuwa msaada wangu. 1
19Alinileta nje mahali penye nafasi tele, 2 akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami. 1
20Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; 2 sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa. 1
21Kwa maana nimezishika njia za Bwana; 2 sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu. 1
22Sheria zake zote zi mbele yangu, 2 wala sijayaacha maagizo yake. 1
23Nimekuwa sina hatia mbele zake, 2 nami nimejilinda nisitende dhambi. 1
24Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu; 2 sawasawa na usafi wa mikono yangu machoni pake. 1
25Kwa yeye aliye mwaminifu, unajionyesha kuwa mwaminifu, 2 kwa asiye na hatia, unajionyesha kutokuwa na hatia. 1
26Kwa aliye mtakatifu, unajionyesha kuwa mtakatifu, 2 lakini kwa aliyepotoka, unajionyesha kuwa mkaidi. 1
27Wewe huwaokoa wanyenyekevu, 2 lakini huwashusha wenye kiburi. 1
28Wewe, Ee Bwana, unaifanya taa yangu iendelee kuwaka; 2 Mungu wangu hulifanya giza langu kuwa mwanga. 1
29Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, 2 nikiwa pamoja na Mungu wangu 2 nitaweza kuruka ukuta. 1
30Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu, 2 neno la Bwana halina dosari. 1 Yeye ni ngao kwa wote 2 wanaokimbilia kwake. 1
31Kwa maana ni nani aliye Mungu 2 zaidi ya Bwana? 1 Ni nani aliye Mwamba 2 isipokuwa Mungu wetu? 1
32Mungu ndiye anivikaye nguvu 2 na kufanya njia yangu kuwa kamilifu. 1
33Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, 2 huniwezesha kusimama mahali palipo juu. 1
34Huifundisha mikono yangu kupigana vita; 2 mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba. 1
35Hunipa ngao yako ya ushindi, 2 nao mkono wako wa kuume hunitegemeza, 2 unajishusha chini ili kuniinua. 1
36Huyapanua mapito yangu, 2 ili miguu yangu isiteleze. 1
37Niliwafuatia adui zangu na nikawapata, 2 sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa. 1
38Niliwaseta hata hawakuweza kuinuka tena; 2 walianguka chini ya miguu yangu. 1
39Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; 2 uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu. 1
40Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, 2 nami nikawaangamiza adui zangu. 1
41Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; 2 walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu. 1
42Niliwaponda kama mavumbi yanayopeperushwa na upepo; 2 niliwamwaga nje kama tope barabarani. 1
43Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu; 2 umenifanya kuwa kiongozi wa mataifa, 2 watu ambao sikuwajua wananitumikia. 1
44Mara wanisikiapo hunitii, 2 wageni hunyenyekea mbele yangu. 1
45Wote wanalegea, 2 wanatoka katika ngome zao wakitetemeka. 1
46Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! 2 Atukuzwe Mungu Mwokozi wangu! 1
47Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, 2 awatiishaye mataifa chini yangu, 2
48aniokoaye na adui zangu. 1 Uliniinua juu ya adui zangu; 2 uliniokoa toka kwa watu wajeuri. 1
49Kwa hiyo nitakusifu katikati ya mataifa, Ee Bwana; 2 nitaliimbia sifa jina lako. 1
50Humpa mfalme wake ushindi mkuu, 2 huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, 2 kwa Daudi na wazao wake milele.