Psalms 27
1Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu, 2 nimwogope nani? 1 Bwana ni ngome ya uzima wangu, 2 nimhofu nani? 1
2Waovu watakaposogea dhidi yangu 2 ili wanile nyama yangu, 1 adui zangu na watesi wangu watakaponishambulia, 2 watajikwaa na kuanguka. 1
3Hata jeshi linizunguke pande zote, 2 moyo wangu hautaogopa; 1 hata vita vitokee dhidi yangu, 2 hata hapo nitakuwa na ujasiri. 1
4Jambo moja ninamwomba Bwana, 2 hili ndilo ninalolitafuta: 1 niweze kukaa nyumbani mwa Bwana 2 siku zote za maisha yangu, 1 niutazame uzuri wa Bwana 2 na kumtafuta hekaluni mwake. 1
5Kwa kuwa siku ya shida, 2 atanihifadhi salama katika maskani yake, 1 atanificha uvulini mwa hema yake 2 na kuniweka juu kwenye mwamba. 1
6Kisha kichwa changu kitainuliwa 2 juu ya adui zangu wanaonizunguka. 1 Katika maskani yake nitatoa dhabihu kwa kelele za shangwe; 2 nitamwimbia Bwana na kumsifu. 1
7Isikie sauti yangu nikuitapo, Ee Bwana, 2 unihurumie na unijibu. 1
8Moyo wangu unasema kuhusu wewe, 2 “Utafute uso wake!” 2 Uso wako, Bwana “Nitautafuta.” 1
9Usinifiche uso wako, 2 usimkatae mtumishi wako kwa hasira; 2 wewe umekuwa msaada wangu. 1 Usinikatae wala usiniache, 2 Ee Mungu Mwokozi wangu. 1
10Hata kama baba yangu na mama wakiniacha, 2 Bwana atanipokea. 1
11Nifundishe njia yako, Ee Bwana, 2 niongoze katika njia iliyonyooka 2 kwa sababu ya watesi wangu. 1
12Usiniachilie kwa nia za adui zangu, 2 kwa maana mashahidi wa uongo 2 wameinuka dhidi yangu, 2 wakipumua ujeuri. 1
13Nami bado nina tumaini hili: 2 nitauona wema wa Bwana 2 katika nchi ya walio hai. 1
14Mngojee Bwana, 2 uwe hodari na mwenye moyo mkuu, 2 nawe, umngojee Bwana.