Psalms 91
1Yeye akaaye mahali pa salama pake Yeye Aliye Juu Sana, 2 atadumu katika uvuli wake Mwenyezi. + 91:1 Mwenyezi hapa ina maana ya Shaddai kwa Kiebrania. 1
2Nitasema kumhusu Bwana, “Yeye ndiye kimbilio langu na ngome yangu, 2 Mungu wangu, ambaye ninamtumaini.” 1
3Hakika yeye ataniokoa na mtego wa mwindaji, 2 na maradhi ya kuambukiza ya kuua. 1
4Atakufunika kwa manyoya yake, 2 chini ya mbawa zake utapata kimbilio, 2 uaminifu wake utakuwa ngao na kinga yako. 1
5Hutaogopa vitisho vya usiku, 2 wala mshale urukao mchana, 1
6wala maradhi ya kuambukiza 2 yanayonyemelea gizani, 2 wala tauni iharibuyo adhuhuri. 1
7Ijapo watu elfu wataangukia kando yako, 2 kumi elfu mkono wako wa kuume, 2 lakini haitakukaribia wewe. 1
8Utatazama tu kwa macho yako 2 na kuona adhabu ya waovu. 1
9Kama ukimfanya Aliye Juu Sana kuwa makao yako: 2 naam, Bwana ambaye ni kimbilio langu, 1
10basi hakuna madhara yatakayokupata wewe, 2 hakuna maafa yataikaribia hema yako. 1
11Kwa kuwa atawaagiza malaika zake kwa ajili yako, 2 wakulinde katika njia zako zote. 1
12Mikononi mwao watakuinua, 2 ili usijikwae mguu wako kwenye jiwe. 1
13Utawakanyaga simba na nyoka wakali, 2 simba mkubwa na nyoka utawaponda kwa miguu. 1
14Bwana asema, “Kwa kuwa ananipenda, nitamwokoa; 2 nitamlinda, kwa kuwa analikiri Jina langu. 1
15Ataniita, nami nitamjibu; 2 nitakuwa pamoja naye katika taabu, 2 nitamwokoa na kumheshimu. 1
16Kwa siku nyingi nitamshibisha 2 na kumwonyesha wokovu wangu.”