Psalms 7
1Ee Bwana, Mungu wangu, ninakukimbilia wewe, 2 uniokoe na kunikomboa na wote wanaonifuatia, 1
2la sivyo watanirarua kama simba 2 na kunichana vipande vipande, asiwepo wa kuniokoa. 1
3Ee Bwana, Mungu wangu, kama nimetenda haya 2 na kuna hatia mikononi mwangu, 1
4au ikiwa nimemtenda uovu aliye na amani nami, 2 au nimemnyangʼanya adui yangu pasipo sababu, 1
5basi adui anifuatie na kunipata, 2 auponde uhai wangu ardhini 2 na kunilaza mavumbini. 1
6Amka kwa hasira yako, Ee Bwana, 2 inuka dhidi ya ghadhabu ya adui zangu. 2 Amka, Mungu wangu, uamue haki. 1
7Kusanyiko la watu na likuzunguke. 2 Watawale kutoka juu. 2
8Bwana na awahukumu kabila za watu. 1 Nihukumu Ee Bwana, 2 kwa kadiri ya haki yangu, 1 kwa kadiri ya uadilifu wangu, 2 Ewe Uliye Juu Sana. 1
9Ee Mungu mwenye haki, 2 uchunguzaye mawazo na mioyo, 1 komesha ghasia za waovu 2 na ufanye wenye haki waishi kwa amani. 1
10Ngao langu ni Mungu Aliye Juu Sana, 2 awaokoaye wanyofu wa moyo. 1
11Mungu ni mwamuzi mwenye haki, 2 Mungu aghadhibikaye kila siku. 1
12Kama hakutuhurumia, 2 atanoa upanga wake, 2 ataupinda na kuufunga uzi upinde wake. 1
13Ameandaa silaha zake kali, 2 ameweka tayari mishale yake ya moto. 1
14Yeye aliye na mimba ya uovu 2 na achukuaye mimba ya ghasia huzaa uongo. 1
15Yeye achimbaye shimo na kulifukua 2 hutumbukia katika shimo alilochimba mwenyewe. 1
16Ghasia azianzishazo humrudia mwenyewe, 2 ukatili wake humrudia kichwani. 1
17Nitamshukuru Bwana kwa ajili ya haki yake, 2 na nitaliimbia sifa jina la Bwana Aliye Juu Sana.