Psalms · Biblia (Kiswahili)

Psalms 64

1Ee Mungu, unisikie ninapoeleza lalamiko langu, 2 uyahifadhi maisha yangu kutokana na vitisho vya adui. 1

2Unifiche kutokana na shauri la siri la waovu, 2 kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya. 1

3Wananoa ndimi zao kama panga 2 na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha. 1

4Hurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia, 2 humrushia ghafula bila woga. 1

5Kila mmoja humtia moyo mwenzake 2 katika mipango mibaya; 1 huzungumza juu ya kuficha mitego yao, 2 nao husema, “Ni nani ataiona?” 1

6Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema, 2 “Tumebuni mpango mkamilifu!” 2 Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila. 1

7Bali Mungu atawapiga kwa mishale, 2 nao ghafula wataangushwa. 1

8Atageuza ndimi zao wenyewe dhidi yao 2 na kuwaleta kwenye maangamizi; 1 wote wawaonao watatikisa vichwa vyao 2 kwa dharau. 1

9Wanadamu wote wataogopa, 2 watatangaza kazi za Mungu 2 na kutafakari yale aliyoyatenda. 1

10Wenye haki na wafurahi katika Bwana, 2 na wakimbilie kwake; 2 wanyofu wote wa moyo na wamsifu yeye!

← Psalms 63Read In The App, Free →Psalms 65 →

Study Psalms 64

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschCharles SpurgeonScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150