Psalms 116
1Ninampenda Bwana kwa maana amesikia sauti yangu; 2 amesikia kilio changu ili anihurumie. 1
2Kwa sababu amenitegea sikio lake, 2 nitamwita siku zote za maisha yangu. 1
3Kamba za mauti zilinizunguka, 2 maumivu makuu ya kuzimu yalinipata, 2 nikalemewa na taabu na huzuni. 1
4Ndipo nikaliitia jina la Bwana: 2 “Ee Bwana, niokoe!” 1
5Bwana ni mwenye neema na haki, 2 Mungu wetu ni mwingi wa huruma. 1
6Bwana huwalinda wanyenyekevu, 2 nilipokuwa katika shida kubwa, aliniokoa. 1
7Ee nafsi yangu, tulia tena, 2 kwa kuwa Bwana amekuwa mwema kwako. 1
8Kwa kuwa wewe, Ee Bwana, 2 umeniokoa nafsi yangu na mauti, 1 macho yangu kutokana na machozi, 2 miguu yangu kutokana na kujikwaa, 1
9ili niweze kutembea mbele za Bwana, 2 katika nchi ya walio hai. 1
10Niliamini, kwa hiyo nilisema, 2 “Mimi nimeteseka sana.” 1
11Katika taabu yangu nilisema, 2 “Wanadamu wote ni waongo.” 1
12Nimrudishie Bwana nini 2 kwa wema wake wote alionitendea? 1
13Nitakiinua kikombe cha wokovu 2 na kulitangaza jina la Bwana. 1
14Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana 2 mbele za watu wake wote. 1
15Kifo cha watakatifu kina thamani 2 machoni pa Bwana. 1
16Ee Bwana, hakika mimi ni mtumishi wako, 2 mimi ni mtumishi wako, 2 mwana wa mjakazi wako; + 116:16 Au: mwanao mwaminifu. 1 umeniweka huru 2 toka katika minyororo yangu. 1
17Nitakutolea dhabihu ya kukushukuru 2 na kuliita jina la Bwana. 1
18Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana 2 mbele za watu wake wote, 1
19katika nyua za nyumba ya Bwana, 2 katikati yako, ee Yerusalemu. 2 Msifuni Bwana.