Psalms 98
1Mwimbieni Bwana wimbo mpya, 2 kwa maana ametenda mambo ya ajabu; 1 kitanga chake cha kuume na mkono wake mtakatifu 2 umemfanyia wokovu. 1
2Bwana ameufanya wokovu wake ujulikane 2 na amedhihirisha haki yake kwa mataifa. 1
3Ameukumbuka upendo wake 2 na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli; 1 miisho yote ya dunia imeuona 2 wokovu wa Mungu wetu. 1
4Mpigieni Bwana kelele za shangwe, dunia yote, 2 ipaze sauti kwa nyimbo za shangwe na vinanda; 1
5mwimbieni Bwana kwa kinubi, 2 kwa kinubi na sauti za kuimba, 1
6kwa tarumbeta na mvumo wa baragumu za pembe za kondoo dume: 2 shangilieni kwa furaha mbele za Bwana, aliye Mfalme. 1
7Bahari na ivume na kila kiliomo ndani yake, 2 dunia na wote wakaao ndani yake. 1
8Mito na ipige makofi, 2 milima na iimbe pamoja kwa furaha, 1
9vyote na viimbe mbele za Bwana, 2 kwa maana yuaja kuhukumu dunia. 1 Atahukumu dunia kwa haki 2 na mataifa kwa haki.