Psalms 103
1Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. 2 Vyote vilivyomo ndani yangu 2 vilihimidi jina lake takatifu. 1
2Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana, 2 wala usisahau wema wake wote, 1
3akusamehe dhambi zako zote, 2 akuponya magonjwa yako yote, 1
4aukomboa uhai wako na kaburi, 2 akuvika taji ya upendo na huruma, 1
5atosheleza mahitaji yako kwa vitu vyema, 2 ili ujana wako uhuishwe kama wa tai. 1
6Bwana hutenda haki, 2 naye huwapa hukumu ya haki wote wanaoonewa. 1
7Alijulisha Mose njia zake, 2 na wana wa Israeli matendo yake. 1
8Bwana ni mwingi wa huruma na mwenye neema; 2 si mwepesi wa hasira, bali amejaa upendo. 1
9Yeye hatalaumu siku zote, 2 wala haweki hasira yake milele, 1
10yeye hatutendei kulingana na dhambi zetu 2 wala hatupatilizi kwa kadiri ya maovu yetu. 1
11Kama vile mbingu zilivyo juu ya dunia sana, 2 ndivyo wema wake ulivyo mwingi kwa wanaomcha; 1
12kama mashariki ilivyo mbali na magharibi, 2 ndivyo Mungu alivyoziweka dhambi zetu mbali nasi. 1
13Kama baba alivyo na huruma kwa watoto wake, 2 ndivyo Bwana anavyowahurumia wale wanaomcha; 1
14kwa kuwa anajua tulivyoumbwa, 2 anakumbuka kwamba sisi tu mavumbi. 1
15Kuhusu mwanadamu, siku zake ni kama majani, 2 anachanua kama ua la shambani; 1
16upepo huvuma juu yake nalo hutoweka, 2 mahali pake hapalikumbuki tena. 1
17Lakini kutoka milele hata milele 2 upendo wa Bwana uko kwa wale wamchao, 2 nayo haki yake kwa watoto wa watoto wao: 1
18kwa wale walishikao agano lake 2 na kukumbuka kuyatii mausia yake. 1
19Bwana ameweka imara kiti chake cha enzi mbinguni, 2 ufalme wake unatawala juu ya vyote. 1
20Mhimidini Bwana, enyi malaika zake, 2 ninyi mlio mashujaa mnaozitii amri zake, 2 ninyi mnaotii neno lake. 1
21Mhimidini Bwana, ninyi jeshi lake lote la mbinguni, 2 ninyi watumishi wake mnaofanya mapenzi yake. 1
22Mhimidini Bwana, kazi zake zote 2 kila mahali katika milki yake. 1 Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana.