Psalms · Biblia (Kiswahili)

Psalms 26

1Ee Bwana, nithibitishe katika haki, 2 maana nimeishi maisha yasiyo na lawama; 1 nimemtumainia Bwana 2 bila kusitasita. 1

2Ee Bwana, unijaribu, unipime, 2 uuchunguze moyo wangu 2 na mawazo yangu; 1

3kwa maana upendo wako 2 uko mbele yangu daima, 1 nami natembea siku zote 2 katika kweli yako. 1

4Siketi pamoja na watu wadanganyifu, 2 wala siandamani na wanafiki, 1

5ninachukia kusanyiko la watenda mabaya 2 na ninakataa kuketi pamoja na waovu. 1

6Ninanawa mikono yangu kwa kuwa sina hatia, 2 naikaribia madhabahu yako, Ee Bwana, 1

7nikitangaza sifa yako kwa sauti kubwa, 2 huku nikisimulia matendo yako ya ajabu. 1

8Ee Bwana, naipenda nyumba yako mahali unakoishi, 2 mahali ambapo utukufu wako hukaa. 1

9Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda dhambi, 2 wala uhai wangu pamoja na wamwagao damu, 1

10ambao mikononi mwao kuna mipango miovu, 2 ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa. 1

11Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama; 2 nikomboe na unihurumie. 1

12Miguu yangu imesimama katika uwanja tambarare; 2 katika kusanyiko kuu nitamsifu Bwana.

← Psalms 25Read In The App, Free →Psalms 27 →

Study Psalms 26

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschCharles SpurgeonScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150