Psalms 99
1Bwana anatawala, 2 mataifa na yatetemeke; 1 anakalia kiti cha enzi katikati ya makerubi, 2 dunia na itikisike. 1
2Bwana ni mkuu katika Sayuni; 2 ametukuzwa juu ya mataifa yote. 1
3Wanalisifu jina lako ambalo ni kuu na la kuogopwa: 2 yeye ni mtakatifu! 1
4Mfalme ni mwenye nguvu na hupenda haki, 2 wewe umethibitisha adili; 1 katika Yakobo umefanya 2 yaliyo haki na sawa. 1
5Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, 2 na mkaabudu katika mahali pa kuwekea miguu yake; 2 yeye ni mtakatifu. 1
6Mose na Aroni walikuwa miongoni mwa makuhani wake, 2 Samweli alikuwa miongoni mwa walioliitia jina lake; 1 walimwita Bwana, 2 naye aliwajibu. 1
7Alizungumza nao kutoka nguzo ya wingu; 2 walizishika sheria zake na amri alizowapa. 1
8Ee Bwana, wetu, 2 ndiwe uliyewajibu, 1 kwa Israeli ulikuwa Mungu mwenye kusamehe, 2 ingawa uliadhibu matendo yao mabaya. 1
9Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, 2 mwabuduni kwenye mlima wake mtakatifu, 2 kwa maana Bwana Mungu wetu ni mtakatifu.