Psalms 95
1Njooni, tumwimbie Bwana kwa furaha; 2 tumfanyie kelele za shangwe 2 Mwamba wa wokovu wetu. 1
2Tuje mbele zake kwa shukrani, 2 tumtukuze kwa vinanda na nyimbo. 1
3Kwa kuwa Bwana ni Mungu mkuu, 2 mfalme mkuu juu ya miungu yote. 1
4Mkononi mwake mna vilindi vya dunia, 2 na vilele vya milima ni mali yake. 1
5Bahari ni yake, kwani ndiye aliifanya, 2 na mikono yake iliumba nchi kavu. 1
6Njooni, tusujudu, tumwabudu, 2 tupige magoti mbele za Bwana Muumba wetu, 1
7kwa maana yeye ndiye Mungu wetu, 2 na sisi ni watu wa malisho yake, 2 kondoo chini ya utunzaji wake. 1 Kama mkiisikia sauti yake leo, 2
8msiifanye mioyo yenu migumu 2 kama mlivyofanya kule Meriba, + 95:8 Meriba maana yake ni Kugombana. 1 kama mlivyofanya siku ile 2 kule Masa + 95:8 Masa maana yake ni Kujaribiwa. jangwani, 1
9ambapo baba zenu walinijaribu na kunipima, 2 ingawa walikuwa wameyaona matendo yangu. 1
10Kwa miaka arobaini nilikasirikia kizazi kile, 2 nikasema, “Hawa ni taifa ambalo mioyo yao imepotoka, 2 nao hawajazijua njia zangu.” 1
11Hivyo nikatangaza kwa kiapo katika hasira yangu, 2 “Kamwe hawataingia rahani mwangu.”