Psalms 14
1Mpumbavu anasema moyoni mwake, 2 “Hakuna Mungu.” 1 Wameharibika, matendo yao ni maovu kabisa; 2 hakuna hata mmoja atendaye mema. 1
2Bwana anawachungulia wanadamu chini 2 kutoka mbinguni 1 aone kama wako wenye akili, 2 wowote wanaomtafuta Mungu. 1
3Wote wamepotoka, 2 wameharibika wote pamoja, 1 hakuna atendaye mema. 2 Naam, hakuna hata mmoja! 1
4Je, watendao mabaya kamwe hawatajifunza: 2 wale ambao huwala watu wangu 1 kama watu walavyo mkate, 2 hao ambao hawamwiti Bwana? 1
5Wako hapo, wameingiwa na hofu kuu, 2 maana Mungu yupo pamoja na wenye haki. 1
6Ninyi watenda mabaya mnakwamisha mipango ya maskini, 2 bali Bwana ndiye kimbilio lao. 1
7Laiti wokovu wa Israeli 2 ungalikuja kutoka Sayuni! 1 Wakati Bwana arejeshapo 2 wafungwa wa watu wake, 1 Yakobo na ashangilie, 2 Israeli na afurahi!