Psalms · Biblia (Kiswahili)

Psalms 19

1Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu, 2 anga zahubiri kazi ya mikono yake. 1

2Siku baada ya siku zinatoa habari, 2 usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa. 1

3Hakuna msemo wala lugha, 2 ambapo sauti zao hazisikiki. 1

4Sauti yao imeenea duniani pote, 2 nayo maneno yao yameenea 2 hadi miisho ya ulimwengu. 1 Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua, 2

5linafanana na bwana arusi 2 akitoka chumbani mwake, 1 kama shujaa afurahiavyo 2 kukamilisha kushindana kwake. 1

6Huchomoza upande mmoja wa mbingu, 2 na kufanya mzunguko wake 2 hadi upande mwingine. 2 Hakuna kilichojificha joto lake. 1

7Sheria ya Bwana ni kamilifu, 2 ikihuisha nafsi. 1 Shuhuda za Bwana ni za kuaminika, 2 zikimpa mjinga hekima. 1

8Maagizo ya Bwana ni kamili, 2 nayo hufurahisha moyo. 1 Amri za Bwana huangaza, 2 zatia nuru machoni. 1

9Kumcha Bwana ni utakatifu, 2 nako kwadumu milele. 1 Amri za Bwana ni za hakika, 2 nazo zina haki. 1

10Ni za thamani kuliko dhahabu, 2 kuliko dhahabu iliyo safi sana, 1 ni tamu kuliko asali, 2 kuliko asali kutoka kwenye sega. 1

11Kwa hizo mtumishi wako anaonywa, 2 katika kuzishika kuna thawabu kubwa. 1

12Ni nani awezaye kutambua makosa yake? 2 Nisamehe makosa yangu nisiyoyajua. 1

13Mlinde mtumishi wako na dhambi za makusudi, 2 nazo zisinitawale. 1 Ndipo nitakapokuwa sina lawama, 2 wala sitakuwa na hatia ya kosa kubwa. 1

14Maneno ya kinywa changu 2 na mawazo ya moyo wangu, 1 yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, 2 Mwamba wangu na Mkombozi wangu.

← Psalms 18Read In The App, Free →Psalms 20 →

Study Psalms 19

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschCharles SpurgeonScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150