Psalms 21
1Ee Bwana, mfalme huzifurahia nguvu zako. 2 Tazama jinsi ilivyo kuu furaha yake 2 kwa ushindi unaompa! 1
2Umempa haja ya moyo wake 2 na hukumzuilia maombi ya midomo yake. 1
3Ulimkaribisha kwa baraka tele 2 na kumvika taji ya dhahabu safi kichwani pake. 1
4Alikuomba maisha, nawe ukampa, 2 wingi wa siku milele na milele. 1
5Kutokana na ushindi uliompa, utukufu wake ni mkubwa, 2 umeweka juu yake fahari na utukufu. 1
6Hakika umempa baraka za milele, 2 umemfanya awe na furaha 2 kwa shangwe ya uwepo wako. 1
7Kwa kuwa mfalme anamtumaini Bwana; 2 kwa upendo usiokoma wa Aliye Juu Sana hatatikiswa. 1
8Mkono wako utawashika adui zako wote, 2 mkono wako wa kuume utawakamata adui zako. 1
9Wakati utakapojitokeza 2 utawafanya kama tanuru ya moto. 1 Katika ghadhabu yake Bwana atawameza, 2 moto wake utawateketeza. 1
10Utawaangamiza wazao wao kutoka duniani, 2 uzao wao kutoka wanadamu. 1
11Ingawa watapanga mabaya dhidi yako 2 na kutunga hila, hawawezi kufanikiwa, 1
12kwa kuwa utawafanya wakimbie 2 utakapowalenga usoni pao 2 kwa mshale kutoka kwenye upinde wako. 1
13Ee Bwana, utukuzwe katika nguvu zako, 2 tutaimba na kusifu nguvu zako.