Psalms 34
1Nitamtukuza Bwana nyakati zote, 2 sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote. 1
2Nafsi yangu itajisifu katika Bwana, 2 walioonewa watasikia na wafurahi. 1
3Mtukuzeni Bwana pamoja nami, 2 naam, na tulitukuze jina lake pamoja. 1
4Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, 2 akaniokoa kwenye hofu zangu zote. 1
5Wale wamtazamao hutiwa nuru, 2 nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe. 1
6Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, 2 akamwokoa katika taabu zake zote. 1
7Malaika wa Bwana hufanya kituo 2 akiwazunguka wale wamchao, 2 naye huwaokoa. 1
8Onjeni mwone kwamba Bwana ni mwema, 2 heri mtu yule anayemkimbilia. 1
9Mcheni Bwana enyi watakatifu wake, 2 kwa maana wale wamchao 2 hawapungukiwi na chochote. 1
10Wana simba wenye nguvu 2 hutindikiwa na kuona njaa, 1 bali wale wamtafutao Bwana 2 hawatakosa kitu chochote kilicho chema. 1
11Njooni, watoto wangu, mnisikilize, 2 nitawafundisha kumcha Bwana. 1
12Yeyote kati yenu anayependa uzima 2 na kutamani kuziona siku nyingi njema, 1
13basi auzuie ulimi wake na mabaya, 2 na midomo yake kutokana na kusema uongo. 1
14Aache uovu, atende mema, 2 aitafute amani na kuifuatilia. 1
15Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, 2 na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao. 1
16Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu, 2 ili kufuta kumbukumbu lao duniani. 1
17Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, 2 huwaokoa katika taabu zao zote. 1
18Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, 2 na huwaokoa waliopondeka roho. 1
19Mwenye haki ana mateso mengi, 2 lakini Bwana humwokoa nayo yote, 1
20huhifadhi mifupa yake yote, 2 hata mmoja hautavunjika. 1
21Ubaya utamuua mtu mwovu, 2 nao adui za mwenye haki watahukumiwa. 1
22Bwana huwakomboa watumishi wake, 2 yeyote anayemkimbilia yeye 2 hatahukumiwa kamwe.