Psalms 33
1Mwimbieni Bwana kwa furaha, enyi wenye haki; 2 kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo. 1
2Msifuni Bwana kwa kinubi, 2 mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi. 1
3Mwimbieni wimbo mpya; 2 pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe. 1
4Maana neno la Bwana ni haki na kweli, 2 ni mwaminifu kwa yote atendayo. 1
5Bwana hupenda uadilifu na haki; 2 dunia imejaa upendo wake usiokoma. 1
6Kwa neno la Bwana mbingu ziliumbwa, 2 jeshi lao la angani kwa pumzi ya kinywa chake. 1
7Ameyakusanya maji ya bahari 2 kama kwenye chungu; 1 vilindi vya bahari 2 ameviweka katika ghala. 1
8Dunia yote na imwogope Bwana, 2 watu wote wa dunia wamche. 1
9Kwa maana Mungu alisema, na ikawa, 2 aliamuru na ikasimama imara. 1
10Bwana huzuia mipango ya mataifa, 2 hupinga makusudi ya mataifa. 1
11Lakini mipango ya Bwana inasimama imara milele, 2 makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote. 1
12Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao, 2 watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake. 1
13Kutoka mbinguni Bwana hutazama chini 2 na kuwaona wanadamu wote; 1
14kutoka maskani mwake huwaangalia 2 wote wakaao duniani: 1
15yeye ambaye huumba mioyo yao wote, 2 ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda. 1
16Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake; 2 hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake. 1
17Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu, 2 licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa. 1
18Lakini macho ya Bwana yako kwa wale wamchao, 2 kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo, 1
19ili awaokoe na mauti, 2 na kuwahifadhi wakati wa njaa. 1
20Sisi tunamngojea Bwana kwa matumaini, 2 yeye ni msaada wetu na ngao yetu. 1
21Mioyo yetu humshangilia, 2 kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu. 1
22Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, Ee Bwana, 2 tunapoliweka tumaini letu kwako.