Psalms · Biblia (Kiswahili)

Psalms 50

1Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana, 2 asema na kuiita dunia, 1 tangu mawio ya jua 2 hadi mahali pake liendapo kutua. 1

2Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, 2 Mungu anaangaza. 1

3Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, 2 moto uteketezao unamtangulia, 2 akiwa amezungukwa na tufani kali. 1

4Anaziita mbingu zilizo juu, 2 na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake: 1

5“Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, 2 waliofanya agano nami kwa dhabihu.” 1

6Nazo mbingu zinatangaza haki yake, 2 kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu. 1

7“Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, 2 ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: 2 Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu. 1

8Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, 2 au sadaka zako za kuteketezwa, 2 ambazo daima ziko mbele zangu. 1

9Sina haja ya fahali wa banda lako, 2 au mbuzi wa zizi lako. 1

10Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, 2 na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu. 1

11Ninamjua kila ndege mlimani, 2 nao viumbe wa kondeni ni wangu. 1

12Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, 2 kwa maana ulimwengu ni wangu, 2 pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. 1

13Je, mimi hula nyama ya mafahali 2 au kunywa damu ya mbuzi? 1

14Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, 2 timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana, 1

15na uniite siku ya taabu; 2 nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”

16Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: 1 “Una haki gani kunena sheria zangu 2 au kuchukua agano langu midomoni mwako? 1

17Unachukia mafundisho yangu 2 na kuyatupa maneno yangu nyuma yako. 1

18Unapomwona mwizi, unaungana naye, 2 unapiga kura yako pamoja na wazinzi. 1

19Unakitumia kinywa chako kwa mabaya 2 na kuuongoza ulimi wako kwa hila. 1

20Wanena daima dhidi ya ndugu yako 2 na kumsingizia mwana wa mama yako. 1

21Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, 2 ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. 1 Lakini nitakukemea 2 na kuweka mashtaka mbele yako. 1

22“Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, 2 ama sivyo nitawararua vipande vipande, 2 wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa: 1

23Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, 2 naye aiandaa njia yake 2 ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”

← Psalms 49Read In The App, Free →Psalms 51 →

Study Psalms 50

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschCharles SpurgeonScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150